Mimba ya Vera Sidika yamchefua Huddah, awaponda wazazi single

Posted by Martina Birk on Tuesday, August 27, 2024

- Huddah alifichua yuko tayari kuwa mama hata bila ya baba

- Kulingana na naye, njia ya pekee ikiwa atapata mtoto ni kupitia uhusiano dhabiti

- Mwenzake, Vera Sidika karibuni alikuwa amefichua kuwa na ujauzito

Sosholaiti mwenye utata Huddah Monroe, amemsuta vikali Vera Sidika baada ya kufichua kuwa ana ujauzito.

Kupitia ujumbe wa Snapchat ambao TUKO.co.ke imeusoma, Jumatano, Aprili 4, Huddah, amesema yupo radhi kuwa mama.

Tuma neno ‘NEWS’ kwa 40227 ili kupata habari muhimu pindi zinapochipuka

Habari Nyingine: Winnie Mandela aaga dunia

Habari Nyingine: Jamaa anaswa akijifanya mwanamke ndani ya baa, avuliwa nguo (picha)

Kulingana naye, kila mtoto anahitaji kuwa na wazazi wote wawili kwa kuwa hili litahakikisha anapata malezi bora.

Vilevile Huddah anasema, njia ya pekee ikiwa atapata mtoto ni kupitia uhusiano dhabiti utakaohakikisha watoto wake hanapata mapenzi ya wazazi wawili.

Habari Nyingine: Nilikuwa wa kwanza 'kumuonja' Diamond na aliahidi kunioa - Asema mpenzi wa zamani wa Diamond

"Kwa wanaouliza ni kwa nini sina watoto, nasubiri muda wa Mungu," ameandika.

Mwenzake, Vera Sidika karibuni alikuwa amefichua kuwa na ujauzito, na akawahakikishia mashabiki wake kuhusu hali yake hiyo.

Hata alikuwa amedokeza yupo tayari kuthibitisha kwa picha kuhusu ujauzito wake ili wanaomwona muongo waaibike.

Habari Nyingine: Askofu anusurika ‘kichapo’ kanisani Jumapili ya Pasaka

Huddah anaonekana kumpiga vita mwenzake kwa kuwa wawili hao hawajawahi kukubaliana kwa jambo lolote.

Read ENGLISH VERSION

Una maoni? Una habari ambayo ungependa tuichapishe? Tuma ujumbe kwa mhariri: mwangi.muraguri@tuko.co.ke

Subscribe to watch new videos

Chanzo: TUKO.co.ke

ncG1vNJzZmijmajEorTIpaBnrKWgvG%2BvzmeinmdibH10f5NmpKKlkpZ6uq2Mr5yrmV2otqW1yppkspmdmLWmstSaZKGtlJmuqXnAsJipp56Zrm7DwLOYs6FdqLavs8ueZaGsnaE%3D